I am a CHAMPION!

I will conquer what has not been conquered, defeat will not be in my creed,

I will believe what others have doubted,

I will always endeavor the prestige, honor, and respect of my team,

I have trained my mind and my body will follow,

Who am I?

I am a CHAMPION!

Facebook

Monday, October 17, 2011

Thursday, October 6, 2011

Lesson from Steve Jobs of Apple!

“Your time is limited, so don’t waste it living someone else’s life. Don’t be trapped by dogma – which is living with the results of other people’s thinking. Don’t let the noise of other’s opinions drown out your own inner voice. And most important, have the courage to follow your heart and intuition. They somehow already know what you truly want to become. Everything else is secondary.” SJ


Yawezekana ulipofungua ama kuingia kwenye mtandao kufanya lolote lile uliilotaka kufanya leo hii ukakutana na taarifa za kifo cha Steve Jobs, na kama wewe ni mtumiaji wa kompyuta za Apple ama brauza ya safari utakuwa ulikutana na picha ya Bwana huyu ikieleza umri kuzaliwa na kufa kwake.
 

Inawezekana kabisa si wengi wanamfahamu au waliwai kusikia juu ya mtu huyu ambaye leo vyombo vyote vya habari (vya nje) na mitandao vinaanikiza juu ya kifo cha Mbunifu huyu mwenye kuheshimika duniani.

 Bila shaka kama ulikuwa humjui au hukumfahamu hapo kabla leo utakuwa umemfahamu  japo kidogo kupitia kifo chake, sina nia ya kukujuza juu ya msiba huu au umetokeaje na vitu kama hivyo, hapana, nia yangu ni kutaka tujifunze kwa pamoja sisi kama wajasiriamali juu ya mjasiliamali huyu asiyekata tama kirahisi. Jeni funzo gani tunapata kupitia historia ya maisha yake?

 Kama umepata muda kupitia historia yake utakuwa umegundua kuwa haina chochote cha kufanya na mafanikio yake, kwanza hakulelewa na wazazi wake, kwani baada ya kumzaa walimasili (adopted) kwa wazazi wengine, pili, ubunifu wake hauna uhusiano wowote na elimu yake, kwani aliweza kukaa chuo cha ufundi cha gharama wakati huo miezi sita tu ama muhula Mmoja, hakumaliza chuo, aliishi maisha ya kutangatanga na kuvutiwa zaidi na kazi za mafundi umeme wa magari ambayo ndio ilikuwa kazi ya baba yake (sio mzazi).
 
In this rare photograph, you can see how Steve Jobs looked at the lowest point of his career.
It was taken for Andy Hertzfeld’s birthday in April 1993.
From left to right: Mac programmer Andy Hertzfeld, Lisa and Mac programmer Bill Atkinson, Mac programmer and NeXT co-founder Bud Tribble, and Steve

Tunachokiona ni kuwa toka akiwa mdogo alivutiwa na kutamani kujua zaidi juu ya mambo ya vufaa vya umeme, hapa ndipo alipojenga ukaribu na jamaa Mmoja aliyekuwa akifanya kazi kiwanda cha kompyuta HP Wakati huo, Woz akajenga mazoea kwenda kujifunza nyumbani kwa Woz, akajiunga naye na hatimaye  akamua kununua sehemu ya mradi wa Woz wa Apple, akiwa na nia ya kutengeneza kompyuta bora kabisa duniani akiwa na umri wa miaka 20 tu, wawili hao wakiwa na kamtaji kadogo sana, lakini wakiwa ndoto kuuubwa ya kuubadili ulimwengu kiteknolojia walianza ubunifu kufikia ndoto zao. 
“Sometimes when you innovate, you make mistakes. It is best to admit them quickly, and get on with improving your other innovations.” SJ

Steve alianza kutengeza Apple nyumbani kwake na kuzitembeza madukani, waliweza kuuza japo kwa taabu kidogo kwani yao ilikuwa bodhaa mpya na soko limeshikiliwa na IBM, waliamua kuziongezea ubora kwa kuweka program zaidi na hatimaye baada ya muda walifanikiwa kukamata soko na hivyo miaka mine tangu kuanzishwa ikawa ni kampuni kubwa kiasi cha kuingia soko la hisa, mwaka wa tano walitengeneza faida kubwa kufikia Dola million 200, hivyo kuwa Millionea akiwa na miaka 25 tu.


 Haya yalikuwa mafanikio makubwa sana kwa Steve, lakini pia yalikuja yakiwa yameambatana na majaribu yake, kwani kampuni ilianza kufanya vibaya kiasi cha kufikia kufukuzwa katika kampuni aliyoianzisha na kuamua kuuza hisa zake zote na kuendelea na maisha yake, lakini hakuuza maono wala ndoto zake.
 “I’m convinced that about half of what separates the successful entrepreneurs from the non-successful ones is pure perseverance.” SJ
 Hii ilikuwa ni mwaka 1985, steve aliamua kuendeleza ubunifu wake kwa kuanzisha kampuni mbali mbali za kutengezea programu mbali mbali za kompyuta, hata hivyo hazikuweza kufanya vizuri katika soko, miaka takrina tisa ilikuwa migumu kwake, ilifika mahali akakaribia kukata tamaa, hii ilikuwa mwaka 1993, kwa maneno yake anasema “ankle dip shit”.


 Huko msemo usemao “It is always dark before dawn” au ukiona kiza kimezidi kumekaribia kucha, pengine ndio unaoweza elezea mazingira ya kuibuka tena upya  kwa Steve na hatimaye kufikia mafanikio aliyoyoacha nyuma yake.

 Mwishoni mwa mwaka 1993 akiwa bado ana maono yake na ndoto zake zikiwa hazijaathiriwa na mawimbi ya mkwamo wa kibiashara alianza upya kuboresha bidhaa zake na hivyo kujaribu kuziuza upya kwa makampuni na vyuo, aliamua pia kutengeneza programu ya mwanasesere, alijaribu kutaka kuiingiza katika soko la hisa, akawaona wataalamu wa masoko na wachambuzi, walimcheka sana, walimwona kama anayeota ndoto ya mchana, kampuni yake ilikuwa ikifanya vibaya kwa kipindi cha miaka tisa mfululizo.
“I didn’t see it then, but it turned out that getting fired from Apple was the best thing that could have ever happened to me. The heaviness of being successful was replaced by the lightness of being a beginner again, less sure about everything. It freed me to enter one of the most creative periods of my life.” SJ

 Hakukata tamaa, alikuwa na maono ya mbali na zaidi aliamini kuwa INAWEZEKANA, kutokana na kutokata tama kwake kwa jambo analoamini kuwa linawezekana, miaka miwili baadaye 1995 alipata mafanikio makubwa kupitia programu yake iliyokataliwa kwanza na wataaalumu na hivyo kumuingizia Dola Billioni 1.5, ikiwa ni mara tano zaidi ya alizowai kuingiza akiwa na Apple, huo ulikuwa mwanzo wa mafanikio na hatimaye kurudi tena Apple Macntoshi na kuendeleza ndoto yake ya kubadili ulimwengu kupitia teknologia. 
 “You know, I’ve got a plan that could rescue Apple. I can’t say any more than that it’s the perfect product and the perfect strategy for Apple. But nobody there will listen to me.” SJ



Kutokana historia yake nimejifunza mambo mengi sana, hapa chini ni machache tu:-

  • Kufanikiwa katika jambo lolote maishani  hakuna uhusiano na historia yako au hali ya uchumi ya wazazi wako.
  • Kufanikiwa kwako hakuna uhusiano wa moja kwa moja na elimu yako au wazazi wako. 
  • Kufanikiwa hakuna uhusiano na kazi unayofanya bali fikira na ndoto ulizonazo.
  •  Kufukuzwa kazi si mwisho bali ni mwanzo wa kunoa akili na kutumia ubunifu wako kufikia ndoto zako. 
  • Kushindwa (Failure) ni mwalimu mzuri sana maishani. 
  • Kutokutaka tamaa, kung'ang'ania kile unachokiamini pasipo kujali wengine wanasema nini juu yake ndio msingi mkuu wa kutimiza ndoto zako. NK.  

Winners Boulevard 0784 475576, 0716927070.  For comment or ideas

Wednesday, October 5, 2011

Excellence is Habit!



Seeds of Discipline: Excellence Is a Habit

We learn by observation, imitation and repetition.
 
Habits begin as offhand remarks, ideas and images. And then, layer upon layer, through practice, they grow from cobwebs into cables that shackle or strengthen our lives.
 
Habits are like submarines. They run silent and deep.
 
First we make our habits, then our habits make us.
 
Habits are like comfortable beds. They are easy to get into, but difficult to get out of.
 
Winning and Losing are both learned habits.

By Denis Wailey.

Monday, October 3, 2011

Are you working harder or smarter?




Are you working harder or smarter?
 Katika Ulimwengu wa kipato na kujitafutia riziki watu wote tumegawanyika katika makundi makuu manne, Waajiriwa au Waliojiajiri, Wamiliki wa Biashara na Wawekezaji, makundi hayo pia yamegawanyika katika pande kuu mbili, Kushoto na Kulia.

 Upande wa kushoto kuna makundi ya Waajiriwa na Waliojiajiri, upande wa kulia ni Wamiliki wa biashara na Wawekezaji, mgawanyiko huu unatokana na wapi chanzo kikuu cha mtu mapato yake kinakopakina.

 Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali, wasomi na wataalamu wa uchumi duniani, upande wa kushoto (Waajiriwa na waliojiajiri) ndio wenye watu wengi zaidi duniani asilimiam 95%, ndio wenye kipato kidogo zaidi, unalipa kodi nyingi zaidi, ulio masikini, wasio na uhuru na muda, kipato ama kukaa na familia zao, huku asilimia mkubwa wakiwafanyia kazi walio upande wa kulia na kumiliki asilimia 20 ya utajiri wa dunia.

 Lakini upande wa Kulia, Wamiliki wa mifumo ya Biashara na Wawekezaji, ndio upande wenye watu wachache zaidi duniani asilimia 5% tu huku wakimiliki asilimia 80% ya utajiri woote wa dunia, huu ndio upande ambao kipato chao hakitegemei ufanyaji kazi wao moja kwa moja, wanalipa kodi chache, wana uhuru wa kipato, muda na pia kwenda popote watakapo na kufanya kazi na watu wawatakao.

 Upande huu wa kulia unamiliki mifumo ya biashara na pia unatumia pesa kuingiza pesa kwa walio katika kundi la wawekezaji, hawa hawaitaji kuamka kila siku asubui kwenda kutafuta riziki, mifumo waliotengeneza uwawezesha kuwa na uhakika wa kipato hata kama yuko mbugani au ng’ambo na familia wakitalii kwa muda wowote ule.

 Hivyo ukitaka kuwa na uhuru wa kipato, muda, mahali na kujikwamua toka kwenye umasikini pia unabudi kuanza kufikilia njia kukupeleka upande wa kulia, kuwa Mmiliki wa mfumo wa biashara ama Mwekezaji.

 Wakati wa Zama za Viwanda (Industrial Age) karne iliyopita ilikuwa ni ngumu sana kufikilia kuwa mtu wa upande wa kulia angeweza kufanya juhudi au kupata njia kuhamia upande wa Kulia, ilikuwa ni ndoto, kama haukuzaliwa katika familia yenye utajiri basi ulikuwa na uhakika wa kubaki pale ulipo, upande wa Kushoto.
 

Habari njema ni kuwa ni rahisi sana kwa sasa, katika karne hii na Zama za Taarifa/Habari (Information Age) kwa mtu aliye upande wa kushoto kuweza kuhamia upande wa Kulia na kuwa Mmiliki wa mfumo wa Biashara na hatimaye kuwa Mwekezaji, kukua kwa teknolijia ya habari na mawasiliano, kumefanya ama kurahisisha mambo mengi sana, ikiwemo ufanyaji wa biashara, hivi sasa ulimwengu unashuhudia mamilioni ya matajiri wapya kila mwaka, Pual Zane Pilzer, Next Millionaireas,  japo si rahisi sana kama vile mtu awezavyo kupata ajira ya kima cha chini.
 Aina tatu za Madaraja.
Haya nadhani yanafaa kuitwa madaraja, ili mtu aweze kuhama kutoka upande wa kushoto na kuhamia upande wa kulia anaweza kutumia moja ya madaraja haya matatu, lengo kuu likiwa ni kujenga na kumiliki mfumo wa biashara, madaraja hayo ni:-

 1.      Traditional C-type Corporations- Huu ni mfumo wa kawaida wa biashara ama viwanda vya asili ambapo unajenga au kuanzisha biashara yako, mfano Bakhresa, Mengi, Mo Dewji, Mfuruki nk.

2.      Franchises – Hii ni kununua mfumo uliopo tayari na kuendesha, mfano, Coca cola, Steers, Mc Donald, nk

3.      Network Marketing – hapa unanunua mfumo uliopo na kuwa sehemu ya mfumo uliopo tayari.

 Katika mifumo yote mitatu ama madaraja matatu yana nguvu na changamoto zake, changamoto kubwa kabisa katika daraja la 1 na 2 ni mtaji, mtaji mkubwa unaohitajika ili kuanzisha kampuni au kununua biashara itakoyoweza kuajiri watu wasiopungua 500 ili kuweza kuwa katika kundi la Wamiliki wa Mfumo wa Biashara.

 Nguvu pekee iliyopo katika mfumo au daraja la tatu, Network Marketing ni mtaji mdogo unaohitajika kununua na kuwa sehemu ya mtandao mkubwa, makampuni mengi ya biashara ya mtandao utoa bure mafunzo ya biashara, vitendea kazi na nyenzo mbalimbali kumwezesha mtu kufanikiwa katika mfumo huu, huku ukipata fursa ya kuwa na biashara ya kimataifa, na hivyo kuwa Mmiliki wa mfumo huku ukijiandaa kuwa Mwekezaji.

 
“Network Marketing is really the greatest source of grass root capitalism, because it teaches people how to take a small bit of capital, that is your time and build the American dream”  Jim Rhon 

  Daraja hili la Biashara ya Mtandao ndilo linapendekezwa na wanazuoni na wachumi wakubwa duniani, kwani kwa mtaji kidogo wa chini ya dola 1,000 mtu anakuwa mmiliki wa mtandao mkuubwa sana duniani, ukimpa mtu uwezo wa kufanya biashara popote duniani na yeyote pia, ni kama kuwa na duka lililowazi saa 24, siku saba za juma, inamfanya mwanamtandao kufanya kazi kwa bidii na smart na si kutumia nguvu kubwa mno kwa ujira kiduchu. 

"Network Marketing has produced more Millionaires than any other industry in the history of the world” Les Brown 
 

Kwa juhudi binafsi mtu anaweza mafanikio makubwa sana katika kipindi kifupi sana kuliko aina nyingine ya mifumo ya biashara.


 


Wiki ijayo tutaangalia mfumo wa Network Marketing, ni nini na unafanyaje kazi?
 
 Nitwangie au ni email ukiwa na swali lolote au maoni kuhusu makala hizi 0716927070, 0784475576, e.brwebangira@gmail.com

   





   




Subscribe via email

Pata nakala ya mada hizi moja kwa moja katika email yako hapa.

Delivered by FeedBurner

SUCCESS

If these qualities describe you...

1. Self Motivated

2. Highly Ambitious

3. Big Thinker

4. Entrepreneurial

5. Not Willing to Settle for Less

6. Goal Oriented

7. Want to Be Your Own Boss,

8. Want to Live a Life by Design

9. Confident in Making Decisions

10. 200% Committed to change your life within the Next 6-12 Months. You read that right - 200%!!

...then, subscribe to the email ABOVE to contact us ASAP to get:-

• A success—and achievement—oriented articles

• Success quotes to motivate and inspire you

• Special offers on new and best-selling personal achievement resources

• Occasional articles from World renown top experts in personal achievement.